ECOWAS yapanga kupiga marufuku mtandio
Mkutano wa ECOWAS uliofanyika mjini Abuja Nigeria umesema mtandio huu wa hadi uso unayumbisha operesheni za maafisa wa usalama katika kuwanasa wahalifu.
Kaskazini mwa Nigeria wapiganaji wa Boko Haram wamekua wakiwatumia wasichana wadogo na wanawake kutekeleza mashambulio ya kujitoa mhanga.
Walipuaji wamekua wakivalia mavazi mapana na kuficha mabomu ndani ya mavazi hayo. Kundi hilo pia limetumia mbinu hiyo katika mataifa ya Cameroon, Chad na Niger ambayo yanashiriki katika operesheni dhidi ya Boko Haram.

0 comments:
Post a Comment