WALIVYOSEMA MAMENEJA KUHUSU KUFUTWA KAZI KWA MOURINHO - ABETIGER UPDATES <script async='async' src='//pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js'></script> <!-- Adslinks --> <ins class='adsbygoogle' data-ad-client='ca-pub-9050840540045431' data-ad-format='auto' data-ad-slot='2619472872' style='display:block'></ins> <script> (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({}); </script>

WALIVYOSEMA MAMENEJA KUHUSU KUFUTWA KAZI KWA MOURINHO

Mameneja wa klabu za Ligi Kuu ya Uingereza wameeleza kushangazwa kwao na hatua ya Chelsea kumfuta kazi meneja Jose Mourinho.
Jose Mourinho, 52, alifutwa Alhamisi miezi saba baada ya kuwaongoza kushinda Ligi ya Premia.
Chelsea kwa sasa wamo alama moja tu juu ya eneo la kushushwa daraja baada ya kushindwa mechi tisa kati ya 16 walizocheza ligini msimu huu.
Hivi ndivyo walivyosema mameneja wenzake EPL:
Louis van Gaal - Manchester United:
Image result for van gaal
"Nimeshangaa sana, si jambo nililolitarajia. Ni meneja mzuri sana na mwenye rekodi ambayo hakuna mwingine anayeifikia katika ulimwengu wa soka, lakini hili linawezekana. Siwezi kusema ni nini kilikuwa kinaendelea Chelsea, lakini nimeshangaa.”
Manuel Pellegrini - Manchester City:
Image result for pellegrini
“Ligi ya Premia imempoteza meneja muhimu sana. Labda meneja ninayetofautiana sana naye katika mengi, lakini ukifikiria vingine – yeye si adui wangu.
"Nafikiri Ligi ya Premia itamkosa. Mimi, sina haja kumkosa mtu fulani, lakini ningependelea Ligi ya Premia ikiwa na Mourinho kushinda ikiwa bila Mourinho.”
Alex Neil - Norwich:
Image result for alex neil
"Nguvu ambazo wachezaji wanazo zimeongezeka sana. Kilichofanyika Chelsea kinaonyesha mchezo ulivyo sasa. Klabu zina wachezaji ‘bidhaa’ wa thamani ya mamilioni. Ni rahisi kutimua mmoja kuliko zaidi ya 20.”

Tony Pulis - West Brom:
Image result for tony pulis
"Ndiye meneja bora zaidi ligini kwa sasa. Timu zetu zimekabiliana mara nyingi. Amekuwa mwema kwangu. Nimesikitika.”

About Tiger

Tiger
Recommended Posts × +

0 comments:

Post a Comment